
Umilisi wa FASIHI SIMULIZI
Author: Bin Gitonga (malenga)
Fasihi Simulizi ni sanaa inayotumia mazungumzo na vitendo kisanii ili kuwasilisha maarifa au ujumbe fulani kutoka kizazi kimoja hadi kingine. Kwa ujumla, Fasihi Simulizi ni sanaa inayobuniwa kuwasilishwa na kusambazwa kwa (lugha ya) mdomo, na vyombo vyake vikubwa ni mdomo na sauti ya binadamu katika hali ya kuimba, kusimulia, kuiga, kughani, kutamba na kutega kama vile vitendawili vinavyotegwa kwa hadhira. Kuzuka na kukua kwa sayansi na teknolojia kumeathiri pakubwa maana ya Fasihi hii, Fasihi Simulizi ya jamii ijuayo kusoma na kuandika ni tofauti sana na fasihi simulizi ya jamii isiyo na uandishi, kwa vile imeathiriwa na ujuzi wa kusoma na kuandika na mitindo ya masimulizi yake hayaendi sambamba na mitindo ya masimulizi yasiyoathiriwa na uandishi. Hata hivyo, utamu wa Fasihi Simulizi ungali upo.
Keywords for this book
You can only order 1 ebook at a time
Book summary
Fasihi Simulizi imefasiliwa na wataalamu mbalimbali. Miongoni mwa waalamu hao ni M.M. Mulokozi (1996) anasema Fasihi Simulizi ni fasihi inayotungwa au kubuniwa kichwani na kuwasilishwa kwa hadhira kwa njia ya mdomo na vitendo bila kutumia maandishi. Kamusi ya TUKI (2004) Fasihi Simulizi ni kazi ya fasihi inayohifadhiwa na kurithishwa kutoka kizazi kimoja hadi kingine kwa njia ya mdomo kama vile: hadithi, ngoma na vitendawili. Balisidya (1983) anasema Fasihi Simulizi ni aina ya fasihi ambayo hutumia mdomo katika kuumbwa, kuwasilishwa na kusambazwa kwa wasikilizaji na watumiaji wake. Wanjara (2011) anasema Fasihi Simulizi ni sanaa ambayo vyenzo kuu ya utunzi, uwasilishaji na usambazaji wake ni sauti pamoja na vitendo. Fasihi Simulizi ni sanaa inayotumia mazungumzo na vitendo kisanii ili kuwasilisha maarifa au ujumbe fulani kutoka kizazi kimoja hadi kingine. Kwa ujumla, Fasihi Simulizi ni sanaa inayobuniwa kuwasilishwa na kusambazwa kwa (lugha ya) mdomo, na vyombo vyake vikubwa ni mdomo na sauti ya binadamu katika hali ya kuimba, kusimulia, kuiga, kughani, kutamba na kutega kama vile vitendawili vinavyotegwa kwa hadhira. Kuzuka na kukua kwa sayansi na teknolojia kumeathiri pakubwa maana ya Fasihi hii, Fasihi Simulizi ya jamii ijuayo kusoma na kuandika ni tofauti sana na fasihi simulizi ya jamii isiyo na uandishi, kwa vile imeathiriwa na ujuzi wa kusoma na kuandika na mitindo ya masimulizi yake hayaendi sambamba na mitindo ya masimulizi yasiyoathiriwa na uandishi. Hata hivyo, utamu wa Fasihi Simulizi ungali upo.
Book details
No other books by this author.